Wednesday, 23 November 2016

KULA SALAD NI MUHIMU KWA AFYA


Salad ni muhimu sana katika mwili kwavile ina wingi wa fiber, fiber hupigana na lehamu mwilini. Fiber iliyoko kwenye salad inasababisha kushiba haraka na kula kidogo hivyo kwa wale wanaopenda kupunguza mwili hii husaidia sana. Salad huanza kuliwa kabla ya chakula kikuu  ( main meal). Kula salad kila mara huleta afya kwa wale wasiopenda kuongeza uzito wa mwili. 

 Antioxidant mara kwa mara ukila salad unapata kiwango cha juu cha damu kwavile ya mboga mboga na mboga ina antioxidants kwa wingi na muhimu kama vitamin C,Lycopene, beta carotene na folic acid, antioxidants ina sifa ya kulinda ngozi dhidi ya uzee au kuzeeka.
Na kuna aina mbalimbali za salad inategemea ni ipi unapendelea.
Salad nzuri huleta fat nzuri mwilini, mafuta hayo yanapatikana kwa kuweka parachichi kwa wingi, olive oil katika salad yako husaidia mwili kufyonza phytochemicals nzuri inayotakiwa mwilini. Na salad haina gharama na haihitaji kutengeneza kwa muda mrefu.



KULA SALAD NI MUHIMU KWA AFYA.

Wednesday, 12 October 2016

FAIDA ZA KUTUMIA TUNDA TENDE MWILINI



 Tunda hili la tende au dates kwa  huota sana kwenye maeneo ya jangwa na yenye joto na ardhi kavu isiyotunza maji, yanastawi kwa wingi katika nchi za mashariki ya kati.



Tende ni tunda lenye virutubisho katika mwili na lina faida nyingi sana, lina kiwango cha sukari asili asilimia 60-70, sukari hii haileti madhara ya kisukari kama inavyoaminiwa na wengi

Leo nitaongelea sababu kumi kati ya nyingi za kwanini tutumie tunda la tende, Sababu hizo ni kama ifuatavyo:-

  1. Huongeza nguvu mwilini kutokana na kuwa na sukari ya asili, pia waweza 
  2. tengeneza juisi ya maziwa na tende
  3. Huzuia meno kuoza pia ni tiba kwa wagonjwa wa anemia kutokana na kuwa na madini mengi ya chuma
  4. Kutokana na kuwa na vitamini na madini kwa wingi hupunguza uwezekano wa kupata kiharusi
  5. Huongeza uwezo wa kujamiiana kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha nguvu
  6. Unaweza kutumia kama mbadala wa sukari
  7. Kwa wajawazito , humuongezea nguvu mama 
  8. Huimarisha mifupa kutokana na kuwa na wingi wa madini ya chuma, potassium kwa wingi
  9. Kutokana na kuwa na kamba kamba husaidia mtu kupata choo kilaini na kwa urahisi
  10. Hongeza mwili kwa haraka kwa wale waliokonda hivyo kama huitaji kuongeza mwili usitumie tende kwa kila wakati
  11. Kwa wenye matatizo ya upungufu wa madini ya chuma tende inasaidia kuongeza madini ya chuma kwa kiwango kikubwa.




    **Hizi ni baadhi kati ya sababu nyingi na faida nyingi za kula tende *.

    Sunday, 2 October 2016

    PAMBANA NA KANSA KWA KUTUMIA VIUNGO HIVI

    Kansa au kwa jina lingine unajulikana kama saratani umekuwa ugonjwa unaotesa watu wengi duniani ,kansa kwa kawaida husababishia mwili madhara mengi maana hushambulia tishu za mwili kutokana na kuunda vimbe ( tumor )mbalimbali kwenye mwili. Ila kwa upande wa kansa ya damu ni tofauti maana hapa huzuia utendaji wa kawaida wa damu na kuzifanya seli ziwe na mgawanyiko usio wa kawaida katika damu. Lakini unaweza pamban na kansa kwa kutumia viungo chakula hivi.


    • Kitunguu swaumu
    • Tangawizi
    • Mdalasini
    • Binzari
    • Pilipili


    • UNASUMBULIWA NA MAFUA?

      Mafua yamekuwa yakimpata karibia kila mtu ila kuna baadhi ya watu hupatwa na tatizo la mafua mara kwa mara, hivyo basi kama unaona unasumbuliwa mara kwa mara suluhisho lake ni kuhakikisha unakula kitunguu kibichi mara kwa mara kwa maana katika kitunguu kuna Vitamin C, fiber, sulfur na virutubisho vinginevyo.


      • USISUMBUKE TENA PONA MAFUA KWA HARAKA KWA KUTAFUNA KITUNGUU KIBICHI!!!

      Saturday, 1 October 2016

      PATA MUONEKANO MZURI WENYE KUVUTIA

      Hakika hakuna mtu asiyependa kuwa na muonekano mzuri wa kuvutia. ila muonekano mzuri haupatikani tu hivi hivi hakuna kizuri kisicho na gharama. Gharama ya kuwa na muonekano mzuri na wenye kuvutia ni kula vizuri, kuwa na afya bora, kula kwa kuzingatia kanuni za afya, kufanya mazoezi nk.
      Kwa kula matunda na mbogamboga ni sehemu ya kujipatia afya bora na si bora afya. Lakini kwa kuepuka kula vyakula visivyo na tija katika miili yetu hakika tutapata afya njema. Katika picha hii ni baadhi ya vyakula ambavyo ukivitumia mara kwa mara kwa familia yako utajenga familia yenye afya bora isiyokuwa na magonjwa yatokanayo na kula bila mpangilio.

      • AFYA NI KILA KITU KATIKA MAISHA YAKO HAKIKISHA UNAILINDA KWA KULA VIZURI

      Sunday, 25 September 2016

      VITU VYA KULA KABLA NA BAADA YA MAZOEZI

      Licha ya mazoezi unayofanya kila siku ni muhimu kufahamu vitu vya kula kabla na baada ya mazoezi hayo, maana vyakula hivyo vina mchango muhimu kwa afaya yako. Kwa ajili  ya kufurahia na kupata faida ya mazoezi hayo ambayo mara nyingi huchukua nguvu nyingi ya mwili ni vizuri kuwa mwangalifu ni kiasi gani cha chakula utatumia. Hakikisha kabla ya mazoezi yoyote unapata kiasi kidogo cha chakula kitakachokufanya uwe na nguvu wakati wa mazoezi ili kuimarisha nguvu ya misuli yako ili uweze kuchoma kalori nyingi na kuboresha afya ya mwili wako bila tabu yoyote.

      Hakikisha unakula saa 1-2 kabla ya mazoezi na kisiwe na kalori zaidi ya 300-500 usile chakula mara na kuanza mazoezi. Unaweza ukala ndizi au mkate wa ata (brown bread), oatmeal au viazi vikuu vichache.

      Baada ya mazoezi hakikisha unakula baada ya dk 20-60 ili mwili wako uweze kurudisha virutubisho vilivyotoka wakati wa mazoezi, hakikisha unachanganya vyakula vya wanga vyenye afya na protini vyenye kalori 400.
      Vyakula hivyo ni kama:-

      • Kuku na wali wa kahawia au (Brown rice)
      • Yai na mkate uliochomwa vizuri
      • Lozi na maziwa mgando
      • Chokoleti zisizo na sukari kwa wingi.

      VYAKULA VYA KUVIEPUKA WAKATI UNATAKA KUPUNGUZA UZITO


      Katika kipindi cha kupunguza uzito ni kipindi ambacho unatakiwa kuwa makini sana na vyakula unavyokula, maana kama unafanya diet au mazoezi mara nyingi mara baada ya mazoezi mwili unakuwa na uhitaji wa kula sasa hapo ndio pakuwa makini unajaza nini maana badala ya kupunguza uzito unaweza jikuta unaongezeka kutokana na kutokuwa makini na ulaji na aina ya chakula.

      Wakati wa kipindi cha kupunguza uzito epuka kunywa soda, juice zenye sukari kwa wingi, vinywaji vyenye kalori kwa wingi . Pia epuka kula mikate mweupe maana haina lishe kama mkate wa ata. Vyakula vingine hatarishi katika zoezi la kupunguza uzito ni vyakula vya migahawani kama burger, chips maana vyakula hivi vina wingi wa mafuta.

      VYAKULA 10 VINAVYOWEZA KUONDOA MAFUTA KWENYE TUMBO

      Watu wengi husumbuliwa na ukubwa wa matumbo(vitambi) hata wengine kupelekea kutumia dawa mbalimbali zinazoonekana kwenye kila mtandao zenye madai ya kupunguza tumbo. Hili husumbua watu wote wanawake kwa wanaume limekuwa janga duniani kote ni jinsi gani watu wanaweza kuondoa mafuta yanayosababisha ukubwa wa tumbo, imepelekea hata wengine kufanyiwa oparesheni ambazo zinagharimu pesa nyingi. Leo nimejaribu kuonyesha vyakula kumi tu vinavyoweza kuunguza mafuta hayo kwa urahisi bila kutumia pesa nyingi. Hivyo hapo juu vinavyoonekana kwenye picha yetu ni jibu tosha kwa kuyeyusha mafuta ya tumbo.

      Thursday, 22 September 2016

      VYAKULA VINAVYOWEZA KUPAMBANA NA TATIZO LA CHUNUSI ZA USO

      Kama chunusi limekuwa ni tatizo katika ngozi yako basi leo nimekuletea baadhi ya vyakula ambavyo vinaweza kuwa msaada mkubwa kwako katika kupambana na tatizo la chunusi. Baadhi ya vyakula hivyo ni:-

      1.  vyakula ambavyo vina wingi wa Omega 3s, vyakula vyenye wingi wa Omega 3s ni kama mafuta ya samaki, maharag, jozi, samaki, spinach nk.
      2. Maji. Unywaji wa maji kw awingi husaidia kuondoa tatizo la chunusi
      3. Vitunguu Swaumu na Vitunguu maji
      4. Asali safi mbichi
      5. Mdalasini
      6. Mafuta ya nazi, Maziwa na Maji
      7. Nafaka zisizokobolewa na mchele wa rangi ya kahawia
      8. Broccoli
      9. Maharage
      10. Kuku wa aina zote
      11. Mayai 
      12. Vyakula vya bahari kama samaki
      13. Karanga kwa kiasi kdg zitumike
      14. Parachichi
      15. Zabibu nyekundu
      16. Shamari (ni zao liko kwenye jamii ya karoti)
      17. Nyanya
      18. Tikiti maji
      19. Karoti
      20. Viazi vitamu.


      Monday, 12 September 2016

      SALAD YA UONO KWA AFYA YAKO


      JINSI YA KULA KWA AFYA BORA

      Ili uweze kuwa na afya bora unaweza kuamua kubadili kutoka kwenye kula vyakula vyeupe na kuhamia kula vyakula vya kahawia. Kama sukari ya kahawia, wali wa kahawia, mkate wa kahawia vyote hivi vinapatikana katika maduka makubwa na madogo.
      *ANZA SASA KUJENGA AFYA BORA KWA FAMILIA YAKO*

      MAZOEZI MUHIMU KWA KILA ASUBUHI


      MATUNDA YENYE KUZUIA MAGONJWA KWA HARAKA

       Kazi ya zabibu ni kuboresha nguvu ya ubongo.
       Pistachio ni nzuri kwa kupambana na mafuta yaliyozidi kwenye damu.
       Aprokoti ni tunda lenye kuweza kupambana na unene uliopitiliza unaosababishwa na ugonjwa wa kisukari.
       Kiwi ni tunda linalosaidia mmeng'enyo mzuri wa chakula.
       Tufaha ni tunda linaloongeza kinga ya mwili au mfumo wa kinga mwilini.
       Korosho ni nzuri kwa kushusha shinikizo la damu.
       Lozi ni nzuri kwa kustawisha mfumo wa neva.
       Tikiti maji linasaidia kazi vizuri katika figo.
       Jozi ni nzuri kuliwa kwa maana zinazuia ugonjwa wa moyo kwa kiasi kikubwa.

      KANUNI 7 ZA MAISHA YENYE AFYA BORA

      Kuishi bila kuugua ugua hakika inawezekana kama utafwata kanuni hizi. Zipo kanuni nyingi lakini leo nitaelezea kanuni chache tu ili kukuwezesha kuweza kuishi maisha yenye afya bora.
      Kanuni ya kwanza ni :-

      • Kunywa maji kwa wingi soda kwa uchache sana
      • Pombe kwa uchache kunywa chai kwa wingi
      • Tumia matunda kwa wingi kuliko kiwango cha pipi
      • Mbogamboga kwa wingi nyama kwa kiwango kidogo
      • Muda mwingi tumia kutembea  kuliko kukaa
      • Hakikisha hupati hasira mara kwa mara badala yake uwe mwenye furaha na kicheko
      • Maneno yawe machache muda mwingi utumike kwa matendo au kazi.

      Thursday, 8 September 2016

      VITU HATARISHI KWA UBONGO WETU

       Kujifunika kichwa wakati wa kulala . Inaweza ikaonekana kama kitu cha ajabu kwa uhalisia tunahitaji hewa safi hasa wakati wa kulala hii inasababisha kupunguza kiwango cha kupumua hewa safi.
       Uvutaji wa hewa chafu unapelekea kunyima ubongo hewa safi kwavile ubongo unahitaji sana hewa safi ili ufanye kazi vizuri.
       Kiwango kikubwa cha sukari ni chanzo kimojawapo cha uharibifu kwa ubongo.
       Uvutaji sigara unaharibu kwa kiasi kikubwa ubongo na ina madhara mengi mwilini. Kwa madhara katika ubongo inasababisha ubongo kusinyaa na hata kusababisha madhara ya akili 
       Kukosa mawazo mazuri na vichocheo katika mawazo kunaweza pelekea ubongo kusinyaa kwa kutokuutendea kazi.
       Kutokupata kifungua kinywa kila mara inaharibu mfumo wa sukari mwilini na usipokula ubongo hautapata virutubisho na ni rahisi kuharibiwa.
       Kuongea mara chache kunaharibu ubongo. Kwasababu kuongea sana inasababisha ubongo kufanya kazi vizuri na kuuchangamsha.
       Kukosa usingizi kwa muda mrefu inapunguza afya ya seli za ubongo.
      Kula kupita kiasi inapelekea uzito kuongezeka na kudidimiza ubongo na kupunguza uwezo wa kufikiri.

      VYAKULA UNAVYOWEZA KUCHANGANYA PAMOJA NA VIKAKUPA MATOKEO MAZURI KWA AFYA

       Spinach na limao,mboga za majani zina wingi wa madini ya chuma unapokamulia limao kidogo inasaidia kufyonza madini ya chuma kwa ufanisi zaidi.
       Strwaberries na spinach changanya pamaoja tengeneza salad kama una tatizo la upungufu wa damu kwa mchanganyiko huo wa madini ya chuma kutoka kwa spinach na wingi wa vitamin c kutoka kwenye strwaberries utapata damu kwa wingi.
       Nyanya na mafuta ya mzeituni kwa mchanganyiko huu inasaidia kupunguza kiwango cha mafuta mwilini,shinikizo la damu na ukuaji wa kansa.
       Jibini na yai, mwili unahitaji vitamini D ili kuimarisha mifupa. Kiini cha yai kina vitamin D kwa wingi. Kaanga yai na nyunyizia jibini juu ya yai.
       Mchanganyiko huu wa matunda ya blackberries,blueberries strwaberries na raspberries yakichanganywa pamoja yatakupa lishe ya kutosha sana mwilini.
       Ndizi na maziwa ya mtindi yanafaa kwa kifungua kinywa chako au mara baada ya mazoezi . Ni mchanganyiko wa pottasium inayopatikana kwenye ndizi na protini inayopatikana kweney maziwa mtindi inasaidia kujenga misuli na kujaza amino acid iliyopungua wakati wa mazoezi ya viungo.
      Samaki na unga wenye mchanganyiko wa viungo mbalimbali.Samaki ana madini mengi  na shahamu DHA na EPA vikichanganywa vizuri inasaidia kupunguza hatari ya kupata kansa.

      ZIFAHAMU FAIDA 10 ZA NDIZI MBIVU MWILINI


      Ndizi ni tunda lenye Vitamin C kwa wingi faida nyingi mwilini lakini leo nitazungumzia faida kumi tu.
      1. Ndizi ina uwezo mkubwa wa kuondoa unyongovu au huzuni.
      2. Ina uwezo wa kurekebisha mfumo wa tumbo
      3. Ina uwezo wa kupunguza shinikizo la damu na hatari ya ugonjwa wa moyo
      4. Inasaidia mifupa kuwa imara kabisa
      5. Kwa mtu mmoja kuna uwezekano wa kupunguza au kuacha uvutaji sigara
      6. Inasaidia kuzuia upungufu wa damu mwilini
      7. Inatupatia nguvu kama italiwa kila mara
      8. Kupunguza maumivu wakati wa hedhi
      9. Kutupa nguvu ya ubongo
      10. Kusaidia kuzuia vidonda vya tumbo.











      Banana Nutrition Facts

      Serving Size: 3.5 ounces (100 grams), raw
      % Daily
      Value
      *
      Amt. Per
      Serving
      Calories
      89
          Calories from fat
      3
      Total fat
      0 g
      1%
          Saturated fat
      0 g
      1%
          Trans fat
      Cholesterol
      0 mg
      0%
      Sodium
      1 mg
      0%
      Total Carbohydrate
      23 g
      8%
          Dietary Fiber
      3 g
      10%
          Sugar
      12 g
      Protein
      1 g
      Vitamin A
      1%
      Vitamin C
      15%
      Calcium
      1%
      Iron
      1%
      *Percent Daily Values are based on a 2,000 calorie diet. Your daily values may be higher or lower depending on your calorie

      VYAKULA NA MATUNDA YANAYOFANANIA NA VIUNGO VYETU VYA MWILI