Wednesday, 12 October 2016

FAIDA ZA KUTUMIA TUNDA TENDE MWILINI



 Tunda hili la tende au dates kwa  huota sana kwenye maeneo ya jangwa na yenye joto na ardhi kavu isiyotunza maji, yanastawi kwa wingi katika nchi za mashariki ya kati.



Tende ni tunda lenye virutubisho katika mwili na lina faida nyingi sana, lina kiwango cha sukari asili asilimia 60-70, sukari hii haileti madhara ya kisukari kama inavyoaminiwa na wengi

Leo nitaongelea sababu kumi kati ya nyingi za kwanini tutumie tunda la tende, Sababu hizo ni kama ifuatavyo:-

  1. Huongeza nguvu mwilini kutokana na kuwa na sukari ya asili, pia waweza 
  2. tengeneza juisi ya maziwa na tende
  3. Huzuia meno kuoza pia ni tiba kwa wagonjwa wa anemia kutokana na kuwa na madini mengi ya chuma
  4. Kutokana na kuwa na vitamini na madini kwa wingi hupunguza uwezekano wa kupata kiharusi
  5. Huongeza uwezo wa kujamiiana kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha nguvu
  6. Unaweza kutumia kama mbadala wa sukari
  7. Kwa wajawazito , humuongezea nguvu mama 
  8. Huimarisha mifupa kutokana na kuwa na wingi wa madini ya chuma, potassium kwa wingi
  9. Kutokana na kuwa na kamba kamba husaidia mtu kupata choo kilaini na kwa urahisi
  10. Hongeza mwili kwa haraka kwa wale waliokonda hivyo kama huitaji kuongeza mwili usitumie tende kwa kila wakati
  11. Kwa wenye matatizo ya upungufu wa madini ya chuma tende inasaidia kuongeza madini ya chuma kwa kiwango kikubwa.




    **Hizi ni baadhi kati ya sababu nyingi na faida nyingi za kula tende *.